Star Tv

Maafisa waandamizi katika ikulu ya White House wamesema mswada wa Rais Joe Biden unaolenga kutoa uraia kwa wahamiaji Milioni 11 wasio na vibali nchini Marekani, utawasilishwa bungeni kwa ajili ya majadiliano.

Wabunge wawili wa chama cha Democratic, Linda Sanchez wa jimbo la California na seneta wa New Jersey Bob Mendez watawasilisha mswada huo katika bunge la wawakilishi na seneti.

Mswada huo unatarajiwa kuwapa uraia wahamiaji hao iwapo wataweza kuthibitisha kwamba walikuwa Marekani kuanzia Januari Mosi 2021.

Mswada huo utawanufaisha pia watu watu waliopelekwa Marekani kinyume cha sheria kama watoto na wakakulia nchini humo.

Rais Barack Obama mwaka 2012 alitoa amri ya kulindwa kwa wahamiaji hao na pia kuruhusiwa kufanya kazi ila mrithi wake Donald Trump alitishia kufutilia mbali mpango huo kama sehemu yake ya kupambana na uhamiaji wa aina yoyote ile.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.