Star Tv

Baraza la seneti nchini Marekani limemuondolea mashitaka rais wa zamani wa nchi hiyo Donald Trump, ya kuchochea shambulio baya dhidi ya jengo la bunge.

Hii ni kufuatia vurugu zilizosababishwa na kushindwa kwake katika uchaguzi, Ambapo maseneta 57 walipiga kura ya kumtia hatiani rais huyo wa zamani huku 43 wakikataa mashtaka dhidi yake.

Warepublican saba waliungana na Wademocrat wote kumtia hatiani Trump, lakini idadi hiyo ilikuwa chini sana ya kihunzi cha theluthi mbili iliyohitajika.

Matokeo hayo yameacha migawiko isiyo na utatuzi nchini humo kuhusiana na siasa za Trump zilizosababisha shambulio baya zaidi la ndani dhidi ya mmoja ya mihimili mitatu ya demokrasia ya Marekani.

Ingawa aliondolewa hatia kuhusu shitaka pekee la kuchochea uasi, kesi hii ilishuhudia idadi kubwa zaidi ya maseneta kuwahi kupiga kura kumtia hatiani rais wa chama chao kwa makosa makubwa na madogo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.