Ndege ya usafiri ya jeshi la Ukraine iliyokuwa na abiria watu 28 ilianguka Ijumaa jioni kaskazini mashariki mwa Ukraine.
Ndege hiyo ilikuwa imebeba marubani wa wanafunzi wa chuo cha jeshi la wanaanga, Wizara ya Mambo ya Ndani imesema, na Mamlaka nchini humo imesema watu 22 wamefariki dunia.
Watu wawili walijeruhiwa na kupelekwa hospitalini wakiwa katika hali mbaya, Wizara hiyo imeongeza.
"Miili ya watu 22 imepatikana, watu wawili wamejeruhiwa na zoezi la kutafuta watu wengine wanne linaendelea," mamlaka ya hali za dharura imebaini.
Ndege hiyo ilikuwa katika zoezi la mafunzo, rais Volodimir Zelenski amesema.
Chanzo: rfi Swahili.