#BreakingNews
Mgombea Urais wa Chama Cha UDA William Ruto ametangazwa kushinda kiti cha Urais kwa kuibuka kidedea kwa asilimia 50.49% ya kura ambapo aliyekuwa Mpinzani wake Raila Odinga wa Chama ODM amepata 48.85% ya Kura.
Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati ametangaza matokeo hayo jioni ya leo Agosti 15,2022 ambapo pia amemkabidhi Ruto cheti cha ushindi wa Urais.
Katika hotuba yake ya kwanza Ruto aliyoitoa mara baada ya kutangazwa kushinda kiti cha Urais amewashukuru Wakenya wote waliokuwa katika safari yake ya kugombea Urais na waliojitolea katika hali na mali huku akiwaahidi kwamba atafanya kazi kwa bidii pasipokuwaangusha ili kuisongesha Kenya mbele.