Star Tv

Rais wa Senegal Macky Sall amesema atasafiri hadi Urusi na Ukraine hivi karibuni katika wadhifa wake kama mwenyekiti wa sasa wa Umoja wa Afrika kwa lengo la kuzuru nchi hizo mbili.

Sall amesema kwamba hapo jana jumapili Mei 22,2022 amepokea mamlaka ya wakuu wengine wa nchi wa AU kufanya safari hizo.

Katika mkutano wa pamoja na Kansela wa Ujerumani anayezuru Afrika Olaf Sholz, amesema Afrika ina nia ya kuona amani kupitia mazungumzo kati ya Ukraine na Urusi.

Rais huyo wa Senegal amesema Urusi imetoa mwaliko wa kufanya ziara huku rais wa Ukraine akieleza haja ya kuwasiliana na wakuu wa nchi za Afrika.

Mgogoro wa Urusi na Ukraine umekatiza usambazaji wa nafaka na mafuta ya kupikia, na hivyo kuzidisha uhaba wa chakula hasa katika nchi maskini za Afrika kutokana na kupanda kwa bei na pia bei ya mafuta duniani imepanda kutokana na hilo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.