Rais wa Senegal Macky Sall amesema atasafiri hadi Urusi na Ukraine hivi karibuni katika wadhifa wake kama mwenyekiti wa sasa wa Umoja wa Afrika kwa lengo la kuzuru nchi hizo mbili.
Sall amesema kwamba hapo jana jumapili Mei 22,2022 amepokea mamlaka ya wakuu wengine wa nchi wa AU kufanya safari hizo.
Katika mkutano wa pamoja na Kansela wa Ujerumani anayezuru Afrika Olaf Sholz, amesema Afrika ina nia ya kuona amani kupitia mazungumzo kati ya Ukraine na Urusi.
Rais huyo wa Senegal amesema Urusi imetoa mwaliko wa kufanya ziara huku rais wa Ukraine akieleza haja ya kuwasiliana na wakuu wa nchi za Afrika.
Mgogoro wa Urusi na Ukraine umekatiza usambazaji wa nafaka na mafuta ya kupikia, na hivyo kuzidisha uhaba wa chakula hasa katika nchi maskini za Afrika kutokana na kupanda kwa bei na pia bei ya mafuta duniani imepanda kutokana na hilo.