Star Tv

Wapinzani wa Sudan Kusini wametia saini makubaliano ya kuunda kamandi ya jeshi la pamoja, nguzo muhimu ya makubaliano ya amani yaliyotiwa saini mwaka 2018.

Mkataba huo ulitiwa saini siku ya Jumapili katika mji mkuu, Juba, kufuatia upatanishi wa nchi jirani ya Sudan.

Mvutano kati ya Rais Salva Kiir na Makamu wa Kwanza wa Rais Riek Machar hivi karibuni ulisababisha mapigano kati ya vikosi vyao.

Makubaliano hayo yanaweka masharti ya kuwajumuisha makamanda wa upinzani katika vikosi vya jeshi.

Mrengo wa Rais Kiir utakuwa na uwakilishi wa 60% katika nyadhifa muhimu katika jeshi, polisi na vikosi vya usalama. SPLM-IO ya Bw Machar na makundi mengine ya upinzani yatachukua asilimia 40 iliyobaki.

Upinzani utawasilisha orodha ya makamanda wao ndani ya kipindi cha wiki moja.Itafuatiwa na kuhitimu kwa vikosi vya umoja na kutumwa kwao - ambayo haipaswi kuzidi muda wa miezi miwili, kulingana na mpango huo."Watu wa Sudan Kusini wanatamani amani na amani inahusu usalama na leo tumepiga hatua kubwa katika hilo.

Tumekubaliana kwamba tutasonga mbele,” amesema Meja Jenerali Martin Abucha, aliyewakilisha mrengo wa Bw Machar.

“Ninataka kutoa wito kwa wenzangu kutoka pande nyingine kwamba ni muhimu kunyamazisha milio ya bunduki ili Sudan Kusini ifanikiwe. Kusiwe na mapigano, kusiwe na mashambulizi”.

Aidha Mamlaka ya Kiserikali ya Maendeleo (Igad), imesifu mpango huo kama "mafanikio makubwa".

#ChanzoBBC

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.