Star Tv

Kikundi cha waasi cha eneo la Tigray, Ethiopia kimesema kuwa watu 150 wamekufa kutokana na njaa na kukosekana kwa misaada ya kibinadamu kunafanya hali kuwa mbaya zaidi.

Serikali ya Ethiopia haijajibu lolote kuhusu madai hayo. Lakini awali ilikanusha madai ya Umoja wa Mataifa kuhusu kuweka zuio la misaada kuingia.

Mkuu wa kilimo wa TPLF, Atinkut Mezgebo alisema watu na wanyama wanakufa kutokana na kukosa chakula na dawa na "janga linaweza kuwa kubwa zaidi ya tujuavyo".

Aliiambia BBC Tigrinya kuwa watu wanakufa kutokana na njaa huku wanawake na watoto wakiwa ndio waathirika wakubwa zaidi wa uhaba wa chakula.

Si rahisi kuhakiki madai haya kwa kuwa bado mawasiliano ya simu yamekatwa na intaneti haifanyi kazi Tigray.

Taarifa iliyotolewa na jeshi la Tigrayan siku ya Jumatatu, imesema kuwa kuna baadhi ya vifo vinavyotokea katika kambi na watu kuhama makazi kutokana na mgogoro unaoendelea.

Kwa mujibu wa UN, malori 100 ya chakula yanapaswa kuingia katika eneo hilo kila siku ili kukidhi misaada ya kibinadamu.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.