Star Tv

Mwalimu mmoja wa shule ya msingi ya Gitega nchini Burundi yuko mikononi mwa polisi kwa shutuma za kuwatesa watoto wa shule anaowafundisha.

Mwalimu Espeye Nzeyimana Ecofo Ngobeke, ambaye ni mwalimu wa somo la Kifaransa darasa la nne anasemekana aliwaadhibu wanafunzi 30 kwa kushindwa kujibu maswali aliyowauliza.

Watoto 30 kati ya 45 ni wanafunzi wake waliofeli na akaamua kuwapa adhabu ya kuzunguka uwanja uliojaa mawe kwa magoti.

Magoti yao yalianza kuchubuka na kutokwa damu na ikabidi wapelekwe wote hospitalini kutibiwa.

Afisa elimu katika eneo la Mubuga ilipo shule ya Ngobeke Manirambona Placide, anasema mwalimu huyo yuko mikononi mwa polisi.

"Nzeyimana Esperee alisimamishwa kazi Jumapili asubuhi, na kupelekwa mjini Gitega ambako anasubiri kufikishwa mahakamani"- Alisema Bw. Manirambona Placide.

Taarifa zilizotolewa na polisi zinasema kuwa baada ya kuona jinsi wanafunzi wake walivyoumia, mwalimu huyo hakuonekana tena kazini.

ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.