Star Tv

Hospitali moja ya binafsi jijini Nairobi imesitisha utoaji chanjo ya Covid-19 kutokana na uhaba wake, licha ya serikali kuwa na zaidi ya dozi Milioni moja.

Hospitali ya Aga Khan ilitangaza kwamba itaendelea na huduma za utoaji chanjo wakati itakapopata chanjo zaidi kutoka kwa serikali.

Wizara ya Afya siku ya Jumanne ilisema ni watu 130,575 pekee ambao wamechanjwa kote nchini kufikia sasa, licha ya dozi 806,000 kusambazwa kati ya dozi Milioni 1.12 zilizopo.

Hayo yanajiri baada ya hospitali nyingine ya kibinafsi kuanza kutoza ada ya kupata chanjo ya corona ya Sputnik V ya Urusi, ambayo serikali imetoa tahadhari dhidi ya utumiaji na usambazaji wake.

Serikali ya Kenya imeidhinisha matumizi ya chanjo ya Oxford-AstraZeneca.

Ubalozi wa Urusi nchini Kenya siku ya Jumatatu ilijitenga na uingizaji wa chanjo ya Sputnik V nchini humo.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.