Star Tv

Jeshi la UPDF na polisi nchini Uganda wamewaruhusu wanasheria wa waliokuwa wa mgombea wa kiti cha urais Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine kumtembelea nyumbani kwake Magere anakozuiwa na vikosi hivyo kwa zaidi ya juma moja.

Hii ni baada ya mahakama kuu jana kutoa maamuzi ya ombi la Kyagulanyi na mkewe la kuondolewa kwa vikosi vya jeshi na polisi nyumbani kwake.

Kulingana na mwandishi wa BBC Issaac Mumena, mawakili hao waliruhusiwa kumuona baada ya kukaguliwa kwenye kizuizi cha jeshi kilichowekwa karibu na nyumbani kwake.

Kwa mujibu wa Asumani Basalirwa aliyezungumuza na BBC kwa njia ya simu, iliwachukua muda wa saa kadhaa kuwashawishi wakuu wa jeshi la UPDF na polisi kuweza kumuona mteja wao, lakini baadhi ya watu waliokwenda nao walibaki kwenye kizuizi cha jeshi akiwemo aliyekuwa mgombea wa kiti cha urais Jenerali Henry Tumukunde.

Mwanasheria Basalirwa ameeleza kuwa wamemkuta Bobi Wine akiwa na upungufu wa chakula kutokana na kumzuia kutotoka nje na pia kuwazuia watu kuingia nyumbani kwake ambao wangemletea chakula lakini hali yake kiafya sio mbaya.

“Afya yake ni nzuri, hakuna kitu chochote lakini yeye anataka kitu kimoja tu nacho ni haki yake, anataka apewe uhuru kutoka kwake nyumbani kwenda kufanya kazi yake arudi’’- amesema Asumani Basalirwa.

Masuala muhimu yaliyowapeleka wanasheria hao kwa kiongozi wa chama cha NUP ni pamoja na kushauriana naye jinsi ya kuwasilisha kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 14 mwezi huu wa Januari, yaliyompatia Rais Museveni ushindi wa kuongoza muhula wa sita.

Chanzo na BBC Swahili.

 

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.