Taifa la Malawi limepata pigo kubwa baada ya mawaziri wake wawili kufariki dunia kutokana na ugonjwa wa COVID 19.
Waziri wa habari wa Malawi, Gospel Kazako amethibitisha kuwa mawaziri hao ambao ni Waziri wa serikali za mitaa, Lingson Belekanyama na Waziri wa uchukuzi Sidik Mia wamefariki ndani ya masaa mawili tofauti.
Mwishoni mwa juma, rais wa nchi hiyo Lazarus Chakwera alitoa hotuba maalumu kwa njia ya radio kwa taifa akitoa wito wa kuheshimiwa kwa hatua zilizowekwa za kupambana na maambukizi ya Covid 19 kufuatia ongezeko kubwa katika vifo na maambukizi ya virusi hivyo.
Bwana Chakwera anatarajiwa kutoa hotuba nyingine kwa taifa kwa mujibu wa Kazako.