Star Tv

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed amesema ameanzisha "awamu ya mwisho" ya operesheni ya kijeshi katika jimbo la Tigray kwanza kushambulia mji mkuu wa jimbo hilo, Mekelle.

Waziri Abiy amesema wanajeshi watajaribu wasiwajeruhi raia na ametoa wito kwa watu katika mji huo kusalia majumbani mwao.

Hatua hilo inajiri baada ya muda wa mwisho uliyotolewa kwa wapiganaji wa Tigray kujisalimisha kumalizika siku ya Jumatano.

Chama cha TPLF, ambacho kinadhibiti mji wa Mekelle, kimeapa kuendelea na mapigano.

Aidha, mamia ya watu wameripotiwa kuuawa na maelfu ya wengine kutoroka makwao huku vikosi vya muungano vya Ethiopia vikiteka miji kadhaa ya Tigray kutoka kwa wapiganaji wa TPLF.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.