Star Tv

Mshindi wa tuzo ya Oscar kutoka Kenya Lupita Nyongo ametuma ujumbe wake katika mtandao wa Twitter......

Mshindi wa tuzo ya Oscar kutoka Kenya Lupita Nyongo ametuma ujumbe wake katika mtandao wa Twitter akilalamika kufuatia hatua ya Jarida la Uingereza la Grazia kuhariri picha yake na kuufanya uso wake kuwa nyororo ili kuifanya kuafikia vigezo vya masharti ya urembo ya Ulaya.

Aliisambaza picha iliowekwa katika jarida hilo la mwezi Novemba pamoja na picha alizopiga ambazo zinaonekana akiwa na nywele ndefu.

Nyongo pia alitumia alama ya reli ya #dtm{akimaanisha usiguse nywele zangu} ambacho ni kichwa cha wimbo wa Solange kuhusu watu kuheshimu nywele nyeusi.

Msanii huyo pia alihusika katika mzozo mwengine na jarida jingine la Uingereza , la Evening Standard lilipohariri picha yake katika ukurasa wake wa kwanza.

Jarida hilo baadaye liliomba msamaha.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.