Wizara ya Afya nchini Kenya imetangaza ongezeko la wagonjwa wapya wa corona 28, na wagonjwa hao ni waliopimwa ndani ya saa 24.
Wagonjwa hao wapya walioripotiwa leo Katibu wa Wizara ya Afya Rashid Aman wameifanya idadi ya wagonjwa nchini humo kufikia 700 kutokea wagonjwa 672 ambao walioripotiwa jana Jumapili Mei 10.
Bwana Rashid amesema kwamba kati ya wagonjwa hao wapya 10 wanatokea Mombasa , 9 wanatokea Kajiado na 7 wanatokea Nairobi huku 2 wakitokea Wajir.
Aidha,Wizara hiyo imeripoti uwepo wa kifo cha mgonjwa mmoja na kufanya waliofariki kwa ugonjwa huo mpaka sasa kufikia 23, huku watu 12 wameripotiwa kupona na kufanya idadi ya waliopona kufikia 251.