Star Tv

Kenya imerekodi viwango vya juu vya maambukizi ya virusi vya corona kwa siku baada ya wagonjwa wapya 45 kuthibitishwa leo na kufikisha idadi ya watu 535 waliopatikana na ugonjwa wa Covid -19.

Waziri Kagwe amesema wagonjwa hao wamepatikana baada ya sampuli 1,077 kufanyiwa uchunguzi katika kipindi cha saa 24 zilizopita.

Wagonjwa 29 wote walithibitishwa kuwa wa Nairobi na wanatokea mtaa wa Eastleigh, huku wengine 11 wakiwa ni wa Mombasa na wangine watano wakitokea Wajiri Kaskazini mwa Kenya.

Wizara hiyo pia imetangaza kuwa wagonjwa tisa ambao walikuwa wameambukizwa ugonjwa huo wamepona na kufanya idadi ya waliopona kufikia 182 watu waliopona kutokana na maradhi hayo.

Katika juhudi za kudhibiti maambukizi hayo Kenya bado inaendeleza marufuku ya watu kutotoka nje kuanzia saa moja usiku hadi saa kumi na moja alfajiri.

Marufuku ya usafiri kuingia na kutoka mji kuu wa Nairobi na miji mingine kama vile Madera ,Mombasa, Kilifi na Kwale pwani ya Kenya pia iliwekwa kukabiliana na maambukizi.

Hivi karibuni Wizara ya Afya iliweka masharti mapya ya uendeshaji Migahawa Kenya, ambapo ilisema kuwa itaruhusu Migahawa kuanza kufunguliwa kuanzia saa 11 asubuhi na kufungwa saa 10 jioni.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.