Star Tv

Kenya imeripoti jumla ya visa 411 vya maambukizi ya virusi vya corona Ijumaa ya leo Aprili 01,Mei,2020.

Kwa mujibu wa Waziri wa Afya wa nchi hiyo Bwana Mutahi Kagwe amesema kuwa watu 15 zaidi wamepatikana na virusi bya corona kufuatia uchunguzi wa vipimo vya sampuli 1,434 vilivyofanywa saa 24 zilizopita.

Kenya ambayo ilithibitisha kupata maambukizi ya kwanza ya corona mwezi Machi, imekwishapima sampuli 21,702 kutoka maeneo mbali mbali ya nchi hadi kufikia tarehe 1 Mei.

Waziri huyo wa afya amesema kuwa idadi ya watu waliopona virusi vya corona imepanda na kufikia watu 150 huku sita zaidi wakiruhusiwa kwenda nyumbani baada ya kupona.

Wizara hiyo imesema kuwa idadi ya vifo vilivyosababishwa na Covid-19 imefikia watu 21 baada ya wagonjwa 4 zaidi kufariki dunia.
Kufuatia kutangazwa kwa upimaji wa jumla katika maeneo ya nchi, Wizara imefanya shughuli hiyo katika eneo lenye msongamano wa watu wengi la Kawangware jijini Nairobi siku ya Ijumaa.

Lengo la shughuli hiyo ni kuwabaini na kuwatenga watu walioambukizwa na kutafuta watu waliokutana nao ili kuzuwia kusambaa zaidi kwa virusi vya corona.

Wizara ya Afya na huduma za umma imesema itaanzisha hazina ya kuwasaidia wafanyakazi wa Afya wanaokabiliana na mlipuko wa virusi vya corona huku Wizara ya elimu imesema itachukua hatua kuwalinda wanafunzi kutokana na athari mbaya za hatua zilizochukuliwa kukabiliana na Covid-19.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.