Star Tv

Wananchi wa Kenya wanaendelea  kutoa heshima zao za mwisho kwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Daniel  Arap Moi, aliyefariki dunia wiki iliyopita ambapo leo ni siku ya tatu na ya mwisho tangu wananchi wa Kenya waanze kutoa heshima kwa kiongozi wao.

Mwili wa kiongozi huyo aliyeongoza Kenya kwa miaka 24, umekuwa ukiagwa  katika majengo ya bunge jijini Nairobi kwa siku mbili zilizopita, na leo nafasi imetolewa kwa wananchi wa kawaida kumuaga kiongozi wao.

Shughuli ya kuuaga mwili huo ilianza Jumamosi Februari 8 na kutarajiwa kumalizika leo Jumatatu. Siku ya Jumanne ambapo  kutafanyika misa ya wafu katika uwanja wa kimataifa wa Moi.

Mazishi ya kiongozi huyo wa zamani, yatafanyika siku ya Jumatano nyumbani kwake huko Kabarak katika kaunti ya Nakuru lakini kesho, kutakuwa na ibada ya kitaifa katika uwanja wa Nyayo, inayotarajiwa kuhudhuriwa pia na marais mbalimbali kutoka barani Afrika.

                                                                      Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.