Star Tv

Mwanasiasa wa Kenya William Ruto ataapishwa leo kuwa rais wa tano wa taifa hilo wiki moja baada ya Mahakama ya Juu nchini humo kutupilia mbali shauri la kupinga matokeo ya uchaguzi wa Agosti 9 yaliyompa ushindi.

Ruto ataanza muhula wake wa miaka mitano chini ya changamoto za kupanda kwa bei ya vyakula na nishati pamoja na kiwingu cha ukosefu mkubwa wa ajira na deni la taifa linaongezeka kwa kasi.Mwanasiasa huyo ambaye kwa miaka kumi iliyopita alikuwa makamu wa rais chini ya rais anayondoka madarakani Uhuru Kenyatta, alipata ushindi mwembamba katika uchaguzi wa mwezi Agosti akimbwaga kiongozi wa muda mrefu wa upinzani Raila Odinga.Wakati wa uchaguzi huo, Odinga alikuwa akiungwa mkono na rais Kenyatta ambaye katika miaka ya karibuni alitumbukia kwenye msuguano na Ruto kutokana na sababu za kisiasa.

CHANZO: DW SWAHILI

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.