Star Tv

Mahakama ya Juu Kenya kutoa uamuzi kuhusu uchaguzi wa rais Kenya Mahakama ya juu nchini Kenya itatoa uamuzi wake leo wa kama itaidhinisha au kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa rais wa mwezi uliopita.

Mahakama hiyo yenye majaji saba itatoa uamuzi baada ya wiki iliyopita kusikiliza kwa siku tatu hoja za mawakili wanaowasimamia wagombea wawili wakuu na makundi pinzani ya makamishena wa tume ya uchaguzi. William Ruto, ambaye alitangazwa mshindi wa uchaguzi huo wa Agosti 9, amesema jana kuwa ataheshimu uamuzi wa Mahakama ya Juu kwa sababu Kenya ni nchi inayofuata utawala wa kisheria. Ruto ambaye ni naibu wa rais, alitangazwa mshindi na tume ya uchaguzi kwa kupata asilimia 50.49 dhidi ya asilimia 48.85 ya kiongozi mkongwe Raila Odinga aliyeungwa mkono na Rais Uhuru Kenyatta. Odinga alipinga matokeo hayo na kuwasilisha kesi katika Mahakama ya Upeo akidai kulikuwa na udanganyifu katika mchakato wa kuhesabu kura. Mgombea mwenza wa Odinga, Martha Karua alisema muungano wao wa Azimio One Kenya pia utaheshimu uamuzi wa leo.

CHANZO: DW SWAHILI

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.