Star Tv

Kamishna Mkuu wa Uingereza Jane Marriott ametupilia mbali madai kwamba yeye na nchi yake waliingilia uchaguzi mkuu wa Kenya uliomalizika hivi majuzi.

Marriott alikuwa akijibu madai kwenye mitandao ya kijamii kwamba aliishinikiza tume ya uchaguzi kumtangaza William Ruto kuwa rais mteule baada ya uchaguzi huo.

Baadhi ya watumiaji wa mtandao waliweka picha mtandaoni ambazo hazijathibitishwa zikionesha Marriot akisalimiana na Ruto na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Wafula Chebukati.

Katika mfululizo wa jumbe za twitter, Marriott amesema Uingereza "haiungi mkono wala haina maoni yoyote juu ya wagombeaji au vyama vyovyote katika uchaguzi", na kuyataja madai hayo kuwa "habari potofu".

“Ni nani Wakenya wanamchagua ni suala la watu wa Kenya. Tulikutana na watu kutoka katika nyanja mbalimbali za kisiasa ili kueleza mipango na ushirikiano wa Uingereza na Kenya, ikiwa ni pamoja na taasisi huru,”-Amesema Marriott.

Aidha Marriott amesema Kenya itasalia kuwa mshirika muhimu wa Uingereza, akiongeza kuwa Uingereza iko tayari kuunga mkono viongozi waliochaguliwa na wananchi.

#ChanzoBBC

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.