Mbunge mteule nchini Kenya, Didmas Barasa, amejisalimisha kwa polisi baada ya kutafutwa kwa siku tatu kutokana na tukio la kufyatua risasi na kumuua msaidizi wa mpinzani.
Polisi wanamchukulia Barasa kama mshukiwa wa kisa cha mauaji kilichotokea katika kituo cha kupigia kura siku ya kupiga kura nchini humo.
Polisi wamesema kwa sasa anasaidia mamlaka katika uchunguzi wa tukio hilo.
Aidha Wakili wa mbunge huyo mteule alituma maombi ya dhamana siku ya Alhamisi akisubiri kukamatwa kwake.
#ChanzoBBC