Star Tv

Kiongozi wa Upinzani nchini Kenya Raila Odinga, amesema hali yake ni nzuri na anafuata ushauri wa madaktari kwa kupumzika.

Odinga alifanyiwa uchunguzi wa kawaida wa kimatibabu katika hospitali ya Nairobi siku ya Jumanne hatua iliyozua hofu kuhusu hali yake ya afya.

Madaktari wake wakiongozwa na daktari wake wa kibinafsi, Dkt. David Olunya, walisema Waziri Mkuu huyo wa zamani alikuwa ameshauriwa kupumzika baada ya kuhisi amechoka.

"Raila alienda kufanyiwa uchunguzi wa kawaida wa matibabu katika Hospitali ya Nairobi mnamo Machi 9 baada ya kuhisi uchovu. Amekuwa na kampeni kali na alihitaji kufanyiwa uchunguzi. Hii ilifanyika kwa mafanikio"-Amesema Mtaalamu wa Upasuaji wa Neva Dkt. Olunya, .

Odinga baadaye alitumia mtandao wake wa kijamii wa twitter kuwashukuru wote waliomtakia afueni ya haraka na akiwahakikishia kwamba hali yake ni nzuri.

Chanzo: BBC Swahili.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.