Mkuu wa jeshi la UPDF Jenerali David Muhoozi ameomba msamaha kwa waandishi wa habari kufuatia tukio la jana wakati polisi wa jeshi la UPDF walipowatandika wandishi habari.
Waandishi wa habari hao walikuwa wakimsubiri kiongozi wa chama cha NUP Robert Kyagulanyi, aliyepeleka malalamiko yake kwenye Kamisheni ya haki za binadamu ya Umoja wa mataifa Kololo.
Jenerali David Muhoozi amesema uchunguzi umeanza kwa waliofanya kitendo hicho na hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
Jeshi hilo limesema litalipa gharama za matibabu ya wandishi habari hao.
Waandishi waliojeruhiwa ni Cliff Wamala wa NTV, Josephy Dhabiti NBC,Rashid Nakayi GalaxyFm, Timoth Murungi New Vision, Irene Abaro Monitor, Josephine Namakumbi NBS na Jeff Twesigye NTV.
Jenerali Muhoozi amesema jeshi la UPDF halikuwatuma wanajeshi hao kuwapiga waandishi wa habari.
Aidha, ametoa wito kwa waandishi habari kuwa na vitambulisho vinavyoonesha wakiwa kazini kusaidia kuwatambua na mwisho amesema watafanya mpango kuzungumuza na waandishi wa habari ili kuboresha mahusiano kati ya pande hizo mbili.
Chanzo na BBC Swahili.