Star Tv

Vyama vya upinzani nchini Uganda wameungana kuwa na kituo chao kimoja cha kuhesabu kura katika uchaguzi mkuu.

Vyama hivyo ni NUP, FDC, JEEMA, DP, ANT na mgombea wa kiti cha urais wa kujitegemea Jeneri Henery Tumukunde na Dk.Kiiza Besigye wa serikali ya wananchi

Jukwaa linalojulikana kama UID litahusisha matumizi ya teknolojia na nyenzo zingine kuhakikisha kuwa takwimu za matokeo ya uchaguzi kutoka sehemu mbalimbali nchini Uganda yanahakikiwa ipasavyo.

Hii ina maana kuwa wawakilishi wa vyama vyote vya kisiasa kwenye kituo watashirikiana katika kutoa taarifa kuhusu hali ilivyo kuanzia mwanzo hadi mwisho hasa wakifuatilia vitendo ya ukiukaji wa haki za binadamu.

Mwanasiasa mkongwe Paul Semwogerere aliyewahi kuwania kiti cha urais mwaka 1996 dhidi ya rais ndiye mratibu wa jukwaa hilo.

Daktari Kizza Besigye ambaye amewahi kugombea kiti cha urais mara nne na kushindwa na rais Museveni amenukuliwa akisema kwamba japokuwa upinzani ulishindwa kuungana kuwa na mgombea mmoja, muungano huu ni muhimu sana kuweza kukabiliana na jaribio lolote la wizi wa kura.

Mwenyekiti wa chama cha Jeema ameeleza kuwa wameamua kuwa na kituo chao kwasababu tayari chama tawala cha NRM kimetangaza kuwa watakuwa na kituo chao tofauti na tume ya uchaguzi lakini wenye kutangaza matokeo ni tume ya uchaguzi.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.