Star Tv

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amesema kuwa bado hajaona mtu mwenye uwezo wa kuiongoza Uganda kwa sasa, hivyo ataendelea kuwa madarakani.

Museveni mwenye umri wa miaka 76, ameliongoza taifa la Uganda kwa zaidi ya miongo mitatu.

Akizungumza na viongozi wa chama chake cha National Resistance Movement (NRM) hapo jana, amesema kwamba wapinzani wake hawana vigezo vya kuliongoza taifa la Uganda.

"Ninakasirika sana ninaposikia watu wakiniambia niondoke madarakani,”-Museveni alinukuliwa na vyombo vya habari nchini humo.

Na kuongeza kuwa;“ Wapiga kura ndio wanaoamua, hata nikiondoka nani ataweza kuliongoza taifa hili, nitaondoka tu iwapo kuna mtu wa maana nitakayeona naweza kumuachia Uganda".

Rais Museveni ambaye aliingia madarakani kwa njia ya mapigano ya msituni amekaa madarakani tangu mwaka 1986.

Katika uchaguzi mkuu wa Uganda unaotarajiwa kufanyika Januari 14 mwakani una wagombea 11 wa nafasi ya Urais, 10 kati yao wakitaka kuchukua nafasi ya Yoweri Museveni wa chama tawala cha NRM anayetaka kutetea nafasi yake kwa muhula wa sita.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.