Star Tv

Mwanamfalme wa Uingereza Harry anataka uamuzi wa Wizara ya Mambo ya ndani ya Uingereza, unaomnyima ulinzi wa polisi wakati anapokuwa Uingereza, uangaliwe upya kupitia mahakama.

Mwanamfalme huyo anasema ameazimia kulipia kazi ya polisi wanaomlinda kwa pesa zake binafsi.

Mwanamfalme Harry -The Duke of Sussex, ambaye anaishi Marekani, anataka kuitembelea nchi yao ya Uingereza na familia yake na anajaribu kuhakikisha kunakuwa na usalama wa mke na watoto wake kwa njia hiyo.

"Uingereza itakuwa nyumbani kwa Mwanamfalme Harry na nchi ambako ana matumaini kwamba mke wake na watoto wako salama".

Ukosefu wa ulinzi wa polisi una hatari kubwa ya kibinafsi," Msemaji wake alisema katika taarifa.

The Duke amesisitiza kuwa ulinzi wa kampuni ya kibinafsi inayomlinda nje ya Uingereza hauwezi kuchukua nafasi ya polisi wa ndani wa Uingereza, ambao wanaweza kupata taarifa za ujasusi na mamlaka muhimu ya kisheria.

Ulinzi wa Uingereza wa Mwanamfalme Harry uliondolewa baada ya kuhamia nchini Marekani na familia yake.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.