Mwanamfalme wa Uingereza Harry anataka uamuzi wa Wizara ya Mambo ya ndani ya Uingereza, unaomnyima ulinzi wa polisi wakati anapokuwa Uingereza, uangaliwe upya kupitia mahakama.
Mwanamfalme huyo anasema ameazimia kulipia kazi ya polisi wanaomlinda kwa pesa zake binafsi.
Mwanamfalme Harry -The Duke of Sussex, ambaye anaishi Marekani, anataka kuitembelea nchi yao ya Uingereza na familia yake na anajaribu kuhakikisha kunakuwa na usalama wa mke na watoto wake kwa njia hiyo.
"Uingereza itakuwa nyumbani kwa Mwanamfalme Harry na nchi ambako ana matumaini kwamba mke wake na watoto wako salama".
Ukosefu wa ulinzi wa polisi una hatari kubwa ya kibinafsi," Msemaji wake alisema katika taarifa.
The Duke amesisitiza kuwa ulinzi wa kampuni ya kibinafsi inayomlinda nje ya Uingereza hauwezi kuchukua nafasi ya polisi wa ndani wa Uingereza, ambao wanaweza kupata taarifa za ujasusi na mamlaka muhimu ya kisheria.
Ulinzi wa Uingereza wa Mwanamfalme Harry uliondolewa baada ya kuhamia nchini Marekani na familia yake.
#ChanzoBBC