Star Tv

Kiongozi wa upinzani nchini Belarus Maria Kolesnikova amechana paspoti yake ili kuzuia asifukuzwe nchini humo.

Hali hiyo imetokea wakati maafisa nchini Belarus walipojaribu kumuondoa nchini humo kwa nguvu kiongozi huyo lakini alichukua uamuzi wa kuchana hati yake ya kusafiria akipinga hatua hiyo na kuruka kutoka katika gari aliyokuwemo ndani.

Kolesnikova ambaye ni mmoja wa viongozi wa mwisho ambao bado wako nchini humo wakiongoza maandamano dhidi ya rais Alexander Lukashenko, alikamatwa mpakani baada ya kutoonekana siku ya Jumatatu.

Maafisa wa mpakani wamesema alikuwa anajaribu kutoroka nchini humo lakini wenzake wawili aliokuwa nao ambao waliingia nchini Ukraine wamesema aligoma kufukuzwa nchini humo.

Katika mkutano na waandishi habari kwenye mji mkuu wa Ukraine Kiev, Katibu wa habari wa baraza la uratibu la upinzani, Anton Rodnenkov , pamoja na Katibu wake Mkuu Ivan Kravtsov walielezea kuhusu matukio kadhaa wakati watu hao watatu wakipelekwa mpakani.

CHANZO:DW Swahili.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.