Star Tv

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa mkuu wa mkoa ambaye alikuwa ni Mrisho Gambo.

Rais Magufuli ametengua uteuzi huo leo Juni 19,2020, ambapo mbali na Gambo kutenguliwa kuwa Mkuu wa Mkoa huo pia wapo viongozi wengine wametenguliwa uteuzi wao na ameteua viongozi wengine kushika nafasi zao.

Aliyeishika nafasi ya Mrisho Gambo ni Bw.Idd Kamanta ambaye ndiye atachukua nafasi ya mkuu huyo wa mkoa, Kabla ya uteuzi huo Bw.Kamanta alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Monduli ambapo nafasi yake ya ukuu wa wilaya itajazwa baadaye.

Rais ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Arusha Bw.Gabriel Daqarro na amemteua Bw.Kenan Kihongosi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Kabla ya uteuzi huo Bw.Kihongosi alikuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Iringa.

Pia Rais ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Dkt.Maulid Madeni na amemteua Dkt.John Pima kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Ambapo kabla ya uteuzi huo Dkt.Pima alikuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua Mkoani Tabora.

Aidha, Rais Magufuli amemteua Bw.Jerry Mwanga kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua, Kabla ya Uteuzi huo Bw.Mwanga alikuwa Afisa katikaOfisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wateuzi wote wanatakiwa kuwepo Ikulu ya jijini Dar es Salaam ifikapo Juni 23,2020 saa mbili asubuhi.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.