Star Tv

Raundi ya pili ya fainali za kombe la mataifa ya Afrika, AFCON, itaanza Ijumaa baada ya kumalizika kwa raundi ya kwanza Jumanne na timu 16 kufuzu raundi ya pili zikiongozwa na wenyeji Misri.

Mechi za kwanza Ijumaa zitakuwa baina ya wawakilishi pekee wa Afrika Mashariki, Uganda, dhidi ya Senegal katika uwanja wa Cairo International. Pambano jingine siku hiyo litakuwa baina ya Morocco na Benin katika uwanja wa Al- Salaam mjini Cairo.

Katika raundi hiyo ya pili ambayo itakuwa katika mtindo wa mtoano wenyeji Misri watachuana na Afrika Kusini, DRC itapambana na Madagascar timu ambayo ilikuwa "Cinderella" wa fainali hizi, timu ambayo imeingia katika fainali hizo kwa mara ya kwanza na kushinda kundi lake kwa pointi saba ikiwa ni pamoja na kuifunga timu ngumu ya Nigeria 2-0 katika raundi ya kwanza.

Mechi nyingine za raundi ya pili ni Ghana dhidi ya Tunisia, Mali na Ivory Coast, Algeria dhidi ya Guinea na Nigeria itapambana na Cameroon katika moja ya mechi inayotazamiwa kuwa kali katika raundi ya pili.

Timu za Afrika Mashariki, Tanzania na Burundi zilimaliza mashindano kwa kufungwa mechi zote tatu wakati Kenya ilishinda mechi moja dhidi ya Tanzania na kufungwa na Senegal na Algeria.

Robo fainali za mashindano haya zitaanza Julai 10 na nusu fainali zitakuwa Julai 14 wakati mechi ya fainali ya mwisho itachezwa Julai 19

 

CHANZO: VOA Swahili

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.