Star Tv

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ameagiza vituo vyote vya kutolea huduma za afya vya binafsi na serikali kuweka kituo maalum cha kufanya ufuatiliaji wa magonjwa hasa ya mlipuko ili kuyapatia udhibiti wa uharaka zaidi.

Waziri Ummy ametoa maagizo hayo alipokuwa akifungua mafunzo ya siku nne kwa watoa huduma za afya mkoa wa Dar es salaam yanayolenga kuwajengea uwezo wa kukabiliana na Ugonjwa wa Ebola ambao bado haujathibitika kuwepo nchini. "Amesema kupitia takwimu za Ugonjwa wa ebola nchini Uganda hadi sasa kesi za wagonjwa 132 zimeripotiwa huku idadi ya watumishi wa afya wakiwa 18 kati yao 7 wamefariki, hali inayoilazimu wizara ya afya ya Tanzania kutoa mafunzo hayo kwa wataalumu wake". Amesema Serikali itaendelea kutoa mafunzo ya namna ya kukabiliana na Ugonjwa wa Ebola kwa makundi mbalimbali ikiwemo vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na waganga wa jadi.

Ambapo, mafunzo hayo ya siku nne yatatolewa kwa Halmashauri zote tano za mkoa wa Dar es salaam na kuwafikia watumishi wa afya 3757 kutoka vituo mbalimbali vya afya mkoani humo.

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.