Zaidi ya mataifa 25 na mashirika karibu 20 yamezindua muungano wa kimataifa wa kukabiliana na ukame, wakati wa mkutano wa kimataifa wa mazingira nchini Misri, chini ya uongozi wa Uhispania na Senegal.
Waziri Mkuu wa Uhispania Pendro Sanchez amesema muungano huo utalenga kupambana na ukame popote utakapojitokeza, na kutangaza kuwa nchi yake itachangia kiasi cha awali cha dola milioni tano katika mwaka wa kwanza. Sanchez amesema Ulaya imeshudia ukame mbaya zaidi katika kipindi cha miaka 500 mwaka huu, na Afrika na maeneo mengine ya dunia pia yanakumbwa na uhaba mkubwa wa maji. Ameonya kuwa hakuna nchi moja itayoepuka madhara ya ukame, na kutoa wito kwa jamii ya kimataifa kuunga mkono mkakati huo.
CHANZO: DW SWAHILI