Kesi ya Uhujumu Uchumi namba 2 ya mwaka 2022 inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya ukiongozwa na Wakili Suzan Kimaro uliiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi chini ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Salome Mshasha kuwa upelelezi wa kesi hiyo tayari ulikuwa umekamilika na kuomba tarehe nyingine kwa ajili ya kuwasilisha vibali maalumu kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini DPP.
Mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Moshi Erasto Phili upande wa Mashtaka umeieleza mahakama hiyo kuwa uko tayari kuwasilisha hati zote za kisheria kwa hakimu anayesikiliza kesi hiyo baada ya ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini DPP kuridhia Mahakama hiyo ianze kusikiliza shauri hilo.
Hata hivyo upande wa Utetezi ukiongozwa na Wakili Hellen Mahuna haukuwa na pingamizi lolote baada ya kujiridhisha kuwa Hakimu anayesikiliza Kesi alikuwa na udhuru hadi hapo atakaporejea.
Aidha umeomba shauri hilo kupangwa tarehe ya Karibu kwani mshtakiwa Lengai ole Sabaya kwa sasa anakabiliwa na maradhi ya Moyo. Baada ya kusikiliza pande zote mbili Hakimu Erasto Phili ameamuru shauri hilo kuletwa Mahakamani hapo Novemba 21 ya Mwaka huu na upande wa Mashtaka utawasilisha hati zote za Mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Salome Mshasha. Lengai Ole Sabaya kwa Sasa bado anakabiliwa na shtaka la Uhukumu Uchumi lenye Mashtaka saba ikiwemo, utakatishaji wa Fedha, kuunda genge la kihalifu,Matumizi mabaya ya Madaraka.
Makosa ambayo yanadaiwa aliyatenda huko Bomang’ombe Wilayani Hai Mwaka 2021. Sabaya amerudishwa Rumande hadi Novemba 21 Mwaka huu.