Star Tv

Rishi Sunak sasa atachukua nafasi ya Waziri Mkuu katika wakati mgumu sana kwa uchumi wa taifa hilo, Ambapo bado haijasikika mipango yoyote ya kina kutoka kwake tangu kampeni ya uongozi katika msimu wa joto.

Rishi Sunak amepanda jukwaani kwa hotuba yake ya kwanza kwa umma kama kiongozi wa Tory ambapo ametoa pongezi kwa Liz Truss kwa uongozi wake "wenye heshima" "chini ya hali ngumu nje ya nchi na nyumbani".

Sunak ameahidi kutumikia kwa uadilifu na unyenyekevu nafasi hiyo ya Uwaziri Mkuu, "nitafanya kazi siku baada ya siku kwa ajili ya watu wa Uingereza. Ninaahidi kuwa nitahudumu kwa uadilifu na unyenyekevu," Sunak alisema.

Rishi Sunak amesema Uingereza ni nchi kubwa lakini inakabiliwa na changamoto "kubwa" za kiuchumi.

Wiki saba baada ya kushindwa katika uchaguzi wa viongozi wa Conservative, Rishi Sunak sasa atakabidhiwa ufunguo wa Downing Street.

Sunak ni Waziri Mkuu wa kwanza wa Uingereza mwenye asili ya Asia, na atachukua madaraka huku Uingereza ikikabiliwa na changamoto kubwa za kiuchumi.

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.