Idadi ya watu wanaoshukiwa kuwa na Ebola inaendelea kuongezeka nchini Uganda.
Wizara ya afya imesema kumekuwa na wagonjwa 34 wanaoshukiwa kuambukizwa.
Inaaminika kuwa vifo 21 huenda vilisababishwa na virusi vya Ebola.
Timu za afya nchini humo zinaendelea kufuatilia watu ambao wanaweza kuwa wamekutana nao.
Mlipuko huo ulianza katika wilaya ya kati ya Mubende lakini sasa umeenea katika wilaya mbili jirani.
Bado hakuna kesi zilizothibitishwa katika mji mkuu Kampala.
Huu ni mlipuko wa nne wa Ebolanchi ya Uganda kukabiliwa nao huku nchi jirani zikisema ziko katika hali ya tahadhari.
#ChanzoBBC