Polisi wa Urusi wameripotiwa kuwakamata mamia ya waandamanaji waliokuwa wakiandamana kupinga uamuzi wa Urusi wa kuongeza maelfu ya wanajeshi wa ziada kupigana nchini Ukraine.
Kikundi cha haki za binadamu cha Urusi OVD-Info kiliweka jumla ya idadi ya waliokamatwa kuwa zaidi ya 1,300.
Idadi kubwa zaidi ya waliokamatwa walikuwa raia wa St. Petersburg na Moscow.
Nchini Urusi, mikutano isiyoidhinishwa ni kinyume cha sheria chini ya sheria za kupinga maandamano.
Jana, ofisi ya mwendesha mashitaka ya Moscow ilionya kwamba wito kwenye mtandao wa kujiunga na maandamano yasiyoidhinishwa ya mitaani, au kushiriki katika maandamano hayo, inaweza kusababisha mwananchi kufungwa jela kwa miaka 15.
#ChanzoBBC