Star Tv

Klabu ya Real Madrid imeendeleza rekodi yake ya ushindi msimu huu baada ya kuifunga klabu ya Atletico Madrid katika mchezo wa Derby ya jiji la Madrid.

Ushindi huo umeifanya klabu hiyo iendelee kubaki nafasi ya kwanza katika msimamo wa ligi hiyo iki fuatiwa na mahasimu wao Barcelona huku ikiwa imeweza kushinda mechi zote sita za mwanzoni mwa msimu huu. Klabu hiyo inayonolewa na Carlo Ancelotti imeweza kurudia rekodi yake ya kushinda mechi zote sita za mwanzoni mwa msimu ambapo kwa mara ya mwisho ilifanya hivyo msimu wa mwaka 1987-88. kwa upande mwingine mechi hiyo ilitawaliwa na nyimbo zilizoonekana kuwa za kibaguzi zinazomlenga mchezaji wa Madrid Vinicius Jr zikikosoa aina yake ya ushangiliaji baada ya kufunga goli pia baadhi ya mashabiki walimtupia uchafu mchezaji huyo.

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.