Klabu ya Real Madrid imeendeleza rekodi yake ya ushindi msimu huu baada ya kuifunga klabu ya Atletico Madrid katika mchezo wa Derby ya jiji la Madrid.
Ushindi huo umeifanya klabu hiyo iendelee kubaki nafasi ya kwanza katika msimamo wa ligi hiyo iki fuatiwa na mahasimu wao Barcelona huku ikiwa imeweza kushinda mechi zote sita za mwanzoni mwa msimu huu. Klabu hiyo inayonolewa na Carlo Ancelotti imeweza kurudia rekodi yake ya kushinda mechi zote sita za mwanzoni mwa msimu ambapo kwa mara ya mwisho ilifanya hivyo msimu wa mwaka 1987-88. kwa upande mwingine mechi hiyo ilitawaliwa na nyimbo zilizoonekana kuwa za kibaguzi zinazomlenga mchezaji wa Madrid Vinicius Jr zikikosoa aina yake ya ushangiliaji baada ya kufunga goli pia baadhi ya mashabiki walimtupia uchafu mchezaji huyo.