Star Tv

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula ametoa wito kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA) kuweka mpango wa matumizi ya ardhi katika eneo la Mradi wa wa Chanzo na Kituo cha Tiba ya Maji cha Butimba mkoani Mwanza.

Dkt Mabula ametoa wito huo wakati wa uwekaji jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa chanzo na kituo cha tiba ya Maji Butimba jijini Mwanza uliofanywa na Makamu wa Rais Dkt Phillip Isdori Mpango.

Ameishukuru MWAUWASA kwa kuweka uzio katika eneo linalozunguka mradi huo na kueleza kuwa, eneo hilo likiachwa wazi watu wataingia na ndipo migogoro ya ardhi inapoanza na kusisitiza kuwa mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza imefanya jambo zuri la kuweka uzio.

Aidha amesema pamoja na hatua ya kuwekwa uzio iliyofanywa na mamlaka hiyo lakini mpango wa matumizi bora ya ardhi kwenye eneo hilo ni muhimu ili kujua mahitaji ya huduma mbalimbali.

"Chanzo tunakiona kipo lakini wakiweka mpango wa matumizi mazuri kwenye eneo walilozungushia uzio tutajua tuna uhaba wa nyumba za watumishi zinazoweza kuwepo katika eneo hili na wakazi wake wakawa ni sehemu ya walinzi wa mradi. Uwepo wao utakuwa siyo tu utakuwa umeboresha maeneo lakini tutakuwa tumewapa makazi bora watumishi"- Dkt. Mabula.

Mradi wa ujenzi wa chanzo na kituo cha tiba ya maji Butimba umewekwa jiwe la msingi na Makamu wa Rais Dkt. Phillip Mpango ambapo katika hotuba yake ameagiza mradi huo kukamilika mapema Desemba 2022 ili iwe zawadi ya Krismas kwa wakazi wa jiji la Mwanza na kusisitiza wananchi wanaoishi eneo linalozunguka mradi ni lazima wapewe kipaumbele katika kupatiwa huduma ya maji.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.