Mwanasiasa wa Kenya William Ruto ataapishwa leo kuwa rais wa tano wa taifa hilo wiki moja baada ya Mahakama ya Juu nchini humo kutupilia mbali shauri la kupinga matokeo ya uchaguzi wa Agosti 9 yaliyompa ushindi.
Ruto ataanza muhula wake wa miaka mitano chini ya changamoto za kupanda kwa bei ya vyakula na nishati pamoja na kiwingu cha ukosefu mkubwa wa ajira na deni la taifa linaongezeka kwa kasi.Mwanasiasa huyo ambaye kwa miaka kumi iliyopita alikuwa makamu wa rais chini ya rais anayondoka madarakani Uhuru Kenyatta, alipata ushindi mwembamba katika uchaguzi wa mwezi Agosti akimbwaga kiongozi wa muda mrefu wa upinzani Raila Odinga.Wakati wa uchaguzi huo, Odinga alikuwa akiungwa mkono na rais Kenyatta ambaye katika miaka ya karibuni alitumbukia kwenye msuguano na Ruto kutokana na sababu za kisiasa.
CHANZO: DW SWAHILI