Star Tv

Kaimu rais wa Sri Lanka Ranil Wickremesinghe ametangaza sheria ya hali ya hatari

Katika juhudi za kutuliza vurugu za umma na kuushughulikia uchumi ulioporomoka wa taifa hilo la kisiwa. Tangazo lililotolewa na serikali yake limesema ni sahihi kuchukua hatua kama hiyo kwa maslahi ya usalama wa watu, na kuhakikisha usambazaji wa mahitaji muhimu kwa jamii. Rais wa Sri Lanka aliyetimuliwa madarakani, Gotabaya Rajapaksa ambaye wiki iliyopita aliikimbia nchi, amesema alifanya kila awezalo kuepusha kusambaratika kwa uchumi wa taifa lake. Wickremesinghe ambaye alikuwa mshirika wa karibu wa Rajapaksa ni miongoni mwa wanaopigiwa upatu kuwania rasmi wadhifa wa rais, ingawa waandamanaji waliomfukuza mtangulizi wake wanataka yeye pia afungashe virago na kuondoka.

CHANZO: DW SWAHILI

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.