Star Tv

Rais wa Marekani Joe Biden alitia saini Sheria ya Kukodisha kwa Mkopo, iliyoundwa ili kurahisisha utaratibu wa kusambaza silaha kwa Ukraine.

Hati hivyo, kipengele hicho kilichopewa jina la "Sheria ya Kukodisha, Kulinda Demokrasia nchini Ukraine ya 2022," iliwasilishwa kwa Bunge la Congress hata kabla ya kuanza kwa uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, Januari mwaka huu.

Mnamo Mei 3, muswada huo uliidhinishwa kwa kura nyingi za Baraza la Wawakilishi la Bunge la Marekani (417 waliunga mkono, 10 walipinga), na kabla ya hapo muswada huo uliidhinishwa na Seneti.

Kwa mujibu wa muswada huo, Rais wa Marekani "anaweza kuidhinisha serikali kukopesha au kukodisha mali ya ulinzi kwa Ukraine na nchi nyingine za Ulaya Mashariki zilizoathiriwa na uvamizi wa Urusi nchini Ukraine ili kusaidia kuimarisha ulinzi wa nchi hizi na kulinda raia dhidi ya mashambulizi yanayoweza kutokea au kuendelea".

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameishukuru Marekani na Biden kwa kufufua mpango wa msaada. "Asante @POTUS na watu wa Marekani kwa kuunga mkono Ukraine katika kupigania uhuru na mustakabali wetu," akaunti rasmi ya rais wa Ukraine ilituma ujumbe huo kupitia Twitter.

Wakati wa Vita vya Kidunia vya pili, mmoja wa wapokeaji wakuu wa misaada kama hiyo alikuwa Umoja wa Kisovieti.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alishukuru Marekani na Biden kwa kufufua mpango wa msaada. "Asante @POTUS na watu wa Marekani kwa kuunga mkono Ukraine katika kupigania uhuru na mustakabali wetu," akaunti rasmi ya rais wa Ukrain ilituma ujumbe huo kupitia Tiwtter kwa Kiingereza.

#ChanzoBBC

 

 

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.