Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezitaka taasisi za fedha kubuni mikakati na mbinu zitakazowezesha watanzania wengi zaidi kupata huduma rasmi za kibenki kwa gharama nafuu ili waweze kujiongezea kipato na kujikwamua na umasikini.
Majaliwa ametoa wito huo leo Jumatatu Aprili 11, 2022, katika hafla ya huduma ya Teleza Kidijitali inayotolewa na Benki ya NMB, iliyofanyika jijini Dodoma, Ambapo amezishauri taasisi nyingine za kifedha ziige utoaji wa huduma kwa njia hiyo.
Waziri Mkuu amesema kuwa taasisi hizo hazina budi kuiunga mkono Serikali kwa kubuni mikakati mbalimbali ya kuhamasisha matumizi ya teknolojia katika kukuza uchumi sambamba na kubuni masuluhisho rahisi kwa watumiaji wa kawaida.
Aidha, amesema benki nchini hazina budi kubuni zaidi namna ya kutafuta masuluhusho yaliyo katika sekta za kifedha. “Hongereni NMB kwa ubunifu huu ambao utavutia makundi yote ya kijamii, huduma hii itawezesha wateja wenu kupata huduma ya mikopo kiganjani.”