Star Tv

Benki ya Dunia imesema inatarajia uchumi wa Ukraine utapungua kwa 45% mwaka huu kutokana na vita.

Benki hiyo imetabiri pia kuwa kutakuwa na uharibifu mkubwa wa kiuchumi kuliko uliosababishwa na janga la Covid-19 kote Ulaya mashariki na Asia ya kati, na vikwazo ambavyo havijawahi kushuhudiwa na kusababisha mdororo mkubwa wa uchumi nchini Urusi pia.

Sehemu kubwa ya wafanyakazi wa Ukraine wamelazimika kukimbia na biashara nyingi zimefungwa, huku barabara, viwanda na miundombinu mingine ikiharibiwa.

Benki ya Dunia imebainisha pia juu ya maendeleo ya miaka mingi ya nchi hiyo ikisema yamebatilishwa. "Ukraine ilikuwa chanzo kikuu cha mazao kama vile alizeti na ngano lakini kutokana na mauzo ya nje kusitishwa bei ya vyakula duniani imepanda".

Vikwazo dhidi ya Urusi vinamaanisha kuwa benki ya Dunia inatabiri uchumi wake kupungua zaidi ya 11% mwaka huu.

#ChanzoBBC

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.