Star Tv

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu Balozi, Dkt. Pindi Chana amewataka watumishi wa umma kufanya kazi kwa weledi, ufanisi na kuzingatia taratibu na kanuni zilizopo kwa mujibu wa sheria ili kutoa huduma bora kwa umma.

Dkt. Pindi ametoa kauli hiyo wakati akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Ofisi hiyo na kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya Ofisi ya Waziri mkuu kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 na makadirio ya bajeti mwaka 2022/ 2023 ambapo amewahimiza kuwa wabunifu katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

“Baraza hili linazinduliwa kwa mara ya kwanza hivyo kukutana kwenu hapa iwe sehemu muhimu kwenu ya kuibua ubunifu katika mipango yenu na utekelezaji wa shughuli za ofisi kwa kutumia rasilimali zilizopo tuone namna gani tunaweza kubuni mambo mbalimbali katika mipango yetu kuhakikisha umma unapata huduma stahiki na kwa wakati,”- Amesema Dkt. Pindi.

Amesema kwamba lengo la kuanzishwa kwa mabaraza ya wafanyakazi ni kuongeza ufanisi na tija katika sehemu za kazi, waajiri na wafanyakazi kubadilishana mawazo na kubaini mbinu mbalimbali za kukabiliana na changamoto zinazowakabili.

Aidha amewahimiza watumishi hao kuacha kufanya kazi kwa mazoea na kubadilika kifikra katika utendaji wa kazi akisisitiza upendo, bidii ya kazi, uwajibikaji na uadilifu kulingana na dira ya Ofisi hiyo ya kutoa huduma bora kwa umma na kufikia malengo ya serikali.

Wakati huohuo aliitaka Menejimenti kutataua kero za wafanyakazi kwa wakati hatua itakayosaidia kuleta mabadiliko katika maisha yao na ajira kwa ujumla na kuhakikisha wanakuwa na vitendea kazi vya kutosha vitakavyowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kufanya kazi kwa kujituma.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.