Star Tv

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Innocent Bashungwa ameeleza kuwa ataendelea kusimamia upatikanaji wa miundombinu ya michezo kwenye halmashauri na uhai wa michezo ya UMITASHUMTA na UMISETA mashuleni.

Akizungumza wakati wa kukabidhi Ofisi katika Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Waziri Bashungwa amesema kuwa mambo ambayo walikuwa wakiyasimamia na kuyawekea mikakati yanahitaji ushirikiano wa Wizara mbili kama kuhitaji miundombinu katika halmashauri na kurudisha uhai wa UMISETA na UMITASHUMITA vyote kwa pamoja ambayo vipo chini ya halmashauri ambayo inasimamiwa na TAMISEMI.

Waziri Bashungwa alisema katika kipindi cha mwaka mmoja aliokaa alishirikiana vyema na Naibu Waziri na Katibu Mkuu kuhakikisha Wizara hiyo inaamka kutoka kuwa ya ofisini na kuchangamsha sekta za sanaa, utamaduni na michezo kwa matukio mbalimbali ya kiserikali na kushirikiana na sekta binafsi.

“Hii ni wizara muhimu na ya kimkakati inayosimamia Sekta zinazoajiri vijana wengi, kuburudisha na zinazochangia kwenye pato la Taifa,” alisema Waziri Bashungwa.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.