Star Tv

Vikwazo vikali vya kuzuia kusambaa kwa virusi vya Corona vitaanza kutumika kuanzia leo Jumanne katika majimbo kadhaa ya Ujerumani katika wakati inakabiliwa na wimbi la tano la maambukizo ya ugonjwa wa Covid-19.

Wakazi katika majimbo ya Bavaria, Berlin, Hesse, North Rhine Westphalia, Saarland, Saxony, Schleswig Holstein na Thuringia watakabiliwa na vikwazo hivyo vipya.

Vikwazo hivyo pia vitaanza kutumika katika majimbo mengine huku maafisa wa afya wakijaribu kuzuia kuenea kwa aina mpya ya kirusi cha Omicron.

Viongozi wa majimbo na wale wa serikali kuu walikubaliana kuweka vikwazo zaidi kuanzia Disemba 28, wakati kila jimbo likitwikwa jukumu la kutekeleza vikwazo hivyo.

Maafisa wana wasiwasi juu ya kuongezeka kwa maambukizo mapya kutokana na kirusi cha Omicron, ambacho sasa kimeenea katika majimbo yote 16 ya Ujerumani.

#ChanzoDW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.