Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ilorin nchini Nigeria amezuiliwa na polisi baada ya shutuma za kumpiga mhadhiri wa kike.
Polisi wanasema mwanafunzi huyo alikuwa ameenda kumuona msimamizi kuhusu kazi yake ya mwaka wa mwisho wa mradi ndipo walipofikia hatua ya kuoelewana kulipotokea.
Inadaiwa alimvamia mhadhiri huyo ambaye alipata jeraha kichwani na kuzimia.
Mhadhiri huyo amelazwa katika hospitali isiyojulikana huku mwanafunzi huyo akizuiliwa na polisi.
Msemaji wa chuo hicho Kunle Akogun alithibitisha kisa hicho katika taarifa iliyowasilishwa kwa vyombo vya habari siku ya Jumapili, Ambapo amebainisha pia Mhadhiri huyo anaendelea kupata nafuu.