Star Tv

Jenerali mwandamizi aliyeongoza mapinduzi ya kijeshi hivi karibuni nchini Sudan, Abdel-Fattah Burhan, amejiteua tena kuongoza baraza tawala la mpito, ikiwa ni hatua inayoashiria nia yake ya kuimarisha udhibiti madarakani.

Miongoni mwa walioteuliwa ni watawala waliokuwa kwenye baraza lililopita, ikiwa ni pamoja na Jenerali Mohammed Hamdan Dagalo, ambaye ni mshirika wa karibu wa Burhan aliyetajwa kuwa makamu wa rais, pamoja na majenerali wengine watatu waliorejeshwa.

Viongozi watatu wa makundi ya waasi pia wamejumuishwa kwenye baraza hilo na wawakilishi watano kutoka upande wa kiraia.

Hatua hii inachukuliwa licha ya ahadi zinazotolewa kila mara na watawala wa kijeshi kwamba watarejesha mamlaka kwa serikali ya kiraia, tangu mapinduzi ya Oktoba 25, ambayo yalifuatiwa na maandamano ya wanaounga mkono demokrasia wanaoshinikiza kurejeshwa kwa utawala huo wa kiraia.

#ChanzoDW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.