Star Tv

Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani Anthony Blinken amefanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Sudan Abdalla Hamdok.

Marekani imesema Waziri wake wa mambo ya nje Blinken, amezungumza kwa njia ya simu na Waziri Mkuu huyo aliyeondolewa madarakani, kufuatia Kiongozi huyo Abdalla Hamdok kurejea nyumbani.

Hamdok alikamatwa na kushikiliwa baada ya Jeshi kuendesha mapinduzi ya kiutawala siku ya Jumamosi.

Taarifa iliyotolewa inasema Blinken alikaribisha kuachiliwa kwa Hamdok na akarudia wito wake kwa wanajeshi wa Sudan kuwaachilia huru viongozi wote wa kiraia wanaoshikiliwa.

Maandamano ya kupinga mapinduzi hayo ya kijeshi yanaendelea, huku umati wa watu wakikusanyika katika mji mkuu wa Khartoum kuandamana na kufunga barabara.

Mapema, Jenerali Abdel Fattah al-Burhan alitaka kuhalalisha mapinduzi hayo kwa kuwashutumu makundi ya wanasiasa kwa kuchochea raia dhidi ya vikosi vya jeshi.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.