Star Tv

Jeshi la Uganda limezindua gari la kivita lililoundwa nchini humo.

Kamanda wa vikosi vya ardhi nchini Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ametoa taarifa ya uzinduzi wa gari hilo kwa kuweka picha katika ukurasa wake Twitter,  picha ya kile anachosema kuwa gari la kwanza la kivita kutengenezwa nchini humo.

Anasema "liliundwa na kutengenezwa ncini Uganda", lakini hakutoa maelezo kuhusu muundo na gharama yake.

Gari hilo lililopewa jina la Chui lilizinduliwa na baba yake ambaye pia ndio Amiri Jeshi mkuu wa Taifa hilo, Rais Yoweri Kaguta Museveni.

Jeshi la Uganda mwaka jana lilihusika katika msako mkali dhidi ya maandamano yaliyotikisa mji mkuu, Kampala, kufuatia kukamatwa kwa mgombea urais Bobi Wine.

Maafisa wa Jeshi nchini humo walitetea utumizi wa silaha za moto, wakisema polisi na jeshi walikuwa wakikabiliana na waandamanaji.

#ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.