Star Tv

Mwanasiasa wa upinzani nchini Rwanda ambaye ni mwalimu wa chuo kikuu Christopher Kayumba ameshikiliwa kwa madai ya ubakaji.

Ofisi ya uchunguzi nchini humo imesema imemaliza kufanya uchunguzi na imeshakabidhi mashtaka yake ili yaweze kusikilizwa.

Kiongozi huyo ambaye ni wa chama cha jukwaa la demokrasia yaani Rwandan Platform for Democracy (RPD) alishutumiwa kwa madai ya ubakaji siku chache baada ya kuzindua chama chake.

Kayumba amekanusha madai hayo dhidi yake na kusema wana nia ya kumuharibia taswira yake kwa umma pamoja na ya chama chake.

Aidha, miongoni mwa watu wanaomshutumu ni mwanafunzi wake wa zamani.

#ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.