Mwanasiasa wa upinzani nchini Rwanda ambaye ni mwalimu wa chuo kikuu Christopher Kayumba ameshikiliwa kwa madai ya ubakaji.
Ofisi ya uchunguzi nchini humo imesema imemaliza kufanya uchunguzi na imeshakabidhi mashtaka yake ili yaweze kusikilizwa.
Kiongozi huyo ambaye ni wa chama cha jukwaa la demokrasia yaani Rwandan Platform for Democracy (RPD) alishutumiwa kwa madai ya ubakaji siku chache baada ya kuzindua chama chake.
Kayumba amekanusha madai hayo dhidi yake na kusema wana nia ya kumuharibia taswira yake kwa umma pamoja na ya chama chake.
Aidha, miongoni mwa watu wanaomshutumu ni mwanafunzi wake wa zamani.
#ChanzoBBCSwahili